Header Ads

ad

Vikundi vya Vijana Mngeta Kuwezeshwa na Chama Cha mapinduzi

Kuelekea kuimarisha vikundi vya miradi ya maendeleo katika tarafa ya Mngeta wilayani Kilombero Kikundi cha vijana cha Mngeta Centre kimejiimarisha kwa kupanga safu mpya ya uongozi.

Mngeta centre ni miongoni mwa vikundi vilivyo kwenye mradi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kuvijengea uwezo wa ujasiliamali vikundi vya vijana katika  wilaya ya Kilombero. 

Katib wa Chama cha Mapinduz (CCM) tawi la Mngeta bw.INOSENT LUKOWA amesema kikund hicho cha Mngeta centre bila kujali itikadi kinajumuisha wanachama 64 kwenye kata ya Mngeta.

Bw.Lukowa amesema katika  uchaguzi wa viongozi ambao ulisimamiwa na UVCCM tawi la Mngeta waliochaguliwa kukiimarisha kikundi  ni mwenyekiti  Andrea Masinga, Katib Krisantus Mwampinzi na mtunza hazina Restida Libonge.

Kiongoz wa kamati ya kuratibu mradi huo  Bwana Samweli Kilienyi "Diwani mtoto" amesema mrad huo unaosimamiwa na CCM unaratibiwa na kada wa chama hicho Injinia LAURIAN LUMBANGA ambapo ktk tarafa ya Mngeta jumla ya kata sita zitanufaika.

Bw.Kilienyi amesema CCM itafadhili mradi wa maendeleo kwa vikund 17 kwenye kata sita za tarafa ya Mngeta ambazo ni Igima Mbingu,Mchombe,Mngeta,Chita, na Mlimba.

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.